Wednesday, August 29, 2012

10% ya Tanzania bado haijalimwa

Tanzania ina eneo mraba la hekta 94.3 milioni, ambazo hekta 22 milioni (23%) zimetengwa kwa hifadhi(ikiwa ni eneo kubwa la rasilimali ya ardhi kutengwa kuliko nchi nyingine yeyote Kusini mwa Sahara), ikijumuisha Mbuga za Taifa (hekta 4.2 millioni), hifadhi za wanyama (hekta 7.7 millioni) na hifadhi za misitu (hekta 10.1 millioni).  Eneo lote linalolimwa kwa mwaka ni kama hekta 5.1 millioni ambazo ni asilimia 5 ya uso wa Tanzania.  Ardhi ile nyingine ifaayo kilimo, lakini haijalimwa, ni hekta 10 milioni, na sehemu kubwa ikiwa inatumiwa kulisha mifugo.  Ndani ya hifadhi, kuna hekta nyingine milioni 4 zifaazo kilimo. 
Sheria ya Ardhi 1999, na sheria ya aridhi ya Vijiji 1999
Sheria ya Ardhi na Sheria ya Ardhi ya Vijiji kwa pamoja ni sheria zinazoweka misingi ya kutawala na kusimamia ardhi, kusuluhisha migogoro na mengine yanayohusiana. Utekelezaji wa sheria hizi utahitaji uelimishaji wa washika dau wote
kuhusu haki na wajibu wao, ili waweze kushiriki kikamilifu katika kuitekeleza. 
Wajibu wa Sekta za Umma/Binafsi 
Wizara zote, taasisi za umma na binafsi, ambazo shughuli zake zinahusiana na maendeleo ya ardhi, yabidi zifanye kazi kwa pamoja na Waziri anayesimamia masuala ya ardhi kuhakikisha kunakuweko ufanisi katika utekelezaji wa Sera ya Ardhi. Aidha, Serikali za Mitaa zinatakiwa zifanye kazi kwa pamoja na Waziri anayesimamia ardhi ili uwepo usimamizi sahihi wa ardhi katika maeneo ya mamlaka zao.